Habari
MAFUNZO YA BODI YA SABA YA BODI YA MAJI BONDE LA KATI
Kiongozi mstaafu aliyekuwa Afisa wa Maji Bonde la Rufiji William Mwaluvande ametoa mafunzo Tarehe 19/2/2026 katika ofisi kuu ya Bodi ya Maji Bonde la Kati mjini Singida.
Lengo la mafunzo hayo ni kuipa nguvu, utashi, mbinu, pamoja na uwelewa wa uwajibikaji wa Bodi ya Maji Bonde la Kati katika majukumu ndani ya bodi.
Pia mwaluvande alisema lugha nzuri, pamoja na kujitoa kikamilifu katika majukumu ni mbinu sahihi ya kuleta maendeleo ndani ya Bodi.
Pamoja na kusema hayo aliwataka viongozi wa Bodi kuwapa elimu endelevu watumishi wao pamoja na kuwajengea mawasiliano mazuri na watu wengine kwani hii itawapa uwezo mzuri katika kazi zao za kila siku.

